HII HAPA KAMATI MPYA YA UTENDAJI YANGA


Kamati ya Utendaji kwa kutumia mamlaka iliyopewa na Ibara ya 28 (1) (d) ya Katiba ya Yanga ya mwaka 2010, imefanya uteuzi wa wanachama wafuatao kuwa wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga. 

1. Dkt Athumani Kihamia - Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) 

2. CPA Shija Richard Shija - Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). 

Uteuzi huo unaanza mara moja. 

Katiba hiyo imetoa mamlaka kwa Kamati ya Utendaji ya Yanga kufanya uteuzi wa wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji. 

Uteuzi wa mjumbe mmoja aliyesalia utafanyika baadaye. 

LihatTutupKomentar