SIMBA YANGA WAPATA NEEMA KUTOKA FIFA


Klabu zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania zikiwemo za Simba na Yanga huenda zikapata mgao wa fedha kutoka kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), endapo vitatimiza vigezo vya kupata fungu hilo, imeelezwa.

Taarifa imeeleza kuwa kauli hiyo ilitolewa baada ya FIFA kutangaza itaanza kuipa Tanzania fedha za maendeleo ambazo kwa muda wa mikaa mitatu ilisitisha kuzitoa baada ya TFF kushindwa kuwasilisha ripoti nzuri ya mapato na matumizi.

Aidha, taarifa hiyo imesema kuwa Karia ameeleza fedha hizo zitaelekezwa katika program za vijana na ugawajwi wake kwa vilabu utazingatia utekelezaji ambao utaonekana kuwa wazi.

Karia alisema moja ya vipaumbele vyake alivyoviweka ni kuhakikisha anakuza soka la vijana  ambapo hivi sasa tayari mipango mikakati imeshaanza.


LihatTutupKomentar