ARSENAL YAPOTEA MAN CITY YAENDELEZA KIPIGO TUUU

Mshambuliaji Muargentina, Sergio Aguero akikimbia kishujaa kushangilia baada ya kukamilisha hattrick yake kwa mabao yake ya dakika ya kwanza, 44 na 61 katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Arsenal kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Etihad. Bao pekee la Arsenal limefungwa na Laurent Koscielny dakika ya 11 na kwa ushindi huo, Manchester City inafikisha pointi 59 katika mechi ya 25, sasa ikizidiwa pointi mbili tu na Liverpool wanaongoza ambao hata hivyo wana mechi moja mkononi

LihatTutupKomentar