KARIM BENZEMA AIPA USHINDI MADRID

Mshambuliaji Mfaransa, Karim Benzema akishangilia baada ya kuifungia bao pekee Real Madrid dakika ya 13 akimalizia kazi nzuri ya Lucas Vazquez ikiilaza 1-0 Rayo Vallecano katika mchezo wa La Liga usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid. 
Kwa ushindi huo, Real Madrid inafikisha pointi 29 baada ya kucheza mechi 19, ikibaki nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Liga nyuma ya Atlético Madrid wenye pointi 31 za mechi 16 sawa na Barcelona waliocheza mechi 15

LihatTutupKomentar