YANGA WAANZA USAJIRI NA HUYU HAPA

Yanga waanza na Huyu dirisha dogo kutambulishwa muda wowote

Wakati Ikiwa ni takribani wiki mbili zimesalia ili kuweza kufungwa kwa dirisha dogo la Usajili nchini Tanzania mambo yamezidi kuonekana kwa timu mbalimbali kusajili mashine zao mpya huku wengine wakienda kwa mkopo katika klabu nyingine.

Klabu ya Yanga juzi ilishusha mashine kutoka Congo kwaajili ya kumalizana na uongozi wa Yanga hili likiwa ni pendekezo la Kocha Mwinyi Zahera.

Mchezaji huyo aliwasili juzi usiku huku akipokewa na mwenyekiti wa kamati ya Usajili Yanga Hussein Nyika.

Mchezaji aliyetua nchini ni Ruben Bomba kutoka nchini DR Congo Ambaye anacheza nafasi ya kiungo wa pembeni, Taarifa ambazo kwataunit.co.ke imezipata ni kwamba mchezaji huyo atatambulishwa muda wowote kutoka sasa kama mchezaji wa Yanga na akiwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa dirisha dogo

LihatTutupKomentar