LIONEL MESSI AIVUSHA BARCELONA KUELEKEA 16 _BORA

Lionel Messi akishangilia baada ya kuifungia bao la kwanza Barcelona dakika ya 70 katika ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, PSV kwenye mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Philips mjini Eindhoven.
Bao la pili la Barca lilifungwa na Gerard Pique dakika ya 70, wakati la PSG lilifungwa na Luuk de Jong dakika ya 82.
Kwa matokeo hayo, Barcelona inafuzu hatua ya 16 Bora baada ya kufikisha pointi 13 ikifuatiwa na Tottenham Hotspur na Inter Milan zenye pointi saba kila moja, wakati PSV inashika mkia kwa pointi yake moja

LihatTutupKomentar