Alexs Sanchez AIOKOA MANCHESTER UNTD DAKIKA ZA MWISHOO

Mtokea benchi, Alexis Sanchez akikimbia kushangilia baada ya kuifungia bao la ushindi Manchester United dakika ya 90 ikiilaza Newcastle United 3-2 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Old Trafford. Newcastle ilitangulia kwa mabao ya Kenedy dakika ya saba na Yoshinori Muto dakika ya 10, kabla ya Man United kusawazisha kupitia kwa Juan Mata dakika ya 70 na Anthony Martial dakika ya 76. Sanchez aliingia dakika ya 67 kuchukua nafasi ya Marcus Rashford 

LihatTutupKomentar