TETESI ZA USAJIRI ULAYA LEO step 21



Manchester United na Arsenal wanammezea mate kiungo wa kati wa kikosi cha chini ya miaka 21 wa Hertha Berlin mwenye umri wa miaka 19 Arne Maier. (Sport Bild)

United pia wamejiunga na Tottengam kumg'ang'ania kiungo wa kati wa Ajax Frenkie de Jong. Maajenti walitumwa kumtazama mchezaji huyo mwenye miaka 22 raia wa Uholanzi akicheza dhidi ya Ufaransa mapema mwezi huu. (Sun)

Liverpool wamepata msukakumo wanapoendelea na mikakati ya kumwinda kiungo wa kati wa Cagliari Nicolo Barella, 21, baada ya Juventus kujitoa kutoka mbio za kumsaka raia huyo wa Italia wa kikosi cha chini ya miaka 21. (Calciomercato)

Raul Sanllehi - mkuu mpya wa kandanda huko Arsenal ana matumaini ya kumuunganisha kiungo wa kati wa Sevilla Ever Banega, 30, na meneja Unai Emery huko Emirates. (Sun)

Sanllehi pia anammezea mate mshambuliaji mwenye miaka 22 wa Boca Juniors raia wa Argentina Cristian Pavon. (football.london)

Jurgeni alibadilisha sera za Liverpool za kununua wachezaji kutoka "wingi kwenda ubora" wakati akimtafuta Virgil van Dijk kutoka Southampton. (FourFourTwo)

Mwandishi wa habari Mhispania Guillem Balague anasema mchezaji wa Barcelona raia wa Argentina Lionel Messi, 31, na mwenye miaka 33 wa Juventus raia wa Ureno Cristiano Ronaldo wana mambo mengi pamoja (BBC Radio 5 live Football Daily)

Aliyekuwa mchezaji raia wa Italia Francesco Totti anasema alijaribu kuwashawishi Ronaldo na mshambualiaji raia wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 36, kujiunga naye huko Roma wakati wa siku zake za kucheza. (La Repubblica, via Mail)

LihatTutupKomentar