Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu amesema mechi yao na Simba anaona ya kawaida huku akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kesho.
Kwa takriban siku nne ambazo Yanga imekuwa kambini mkoani Morogoro, imekuwa ikifanya mazoezi ya nguvu na mbinu zaidi kuhakikisha Simba inakufa mapema hapo kesho katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar.
Ajibu ambaye amewahi kucheza Simba, amekuwa gumzo kutokana na kiwango chake kukua na mpaka sasa katika mechi nne alizocheza amefunga bao moja na kutoa pasi za mabao tano.
Mshambuliaji huyo, aliliambia Championi kuwa: “Mechi ni ya kawaida, kikubwa ni kujituma, kwa hiyo mashabiki wasiwe na hofu, dua zao zinahitajika zaidi ili tuweze kupata ushindi kwenye mchezo huu