TETES ZA USAJIRI ULAYA LEO

Wakala wa Kiungo wa Manchester United Paul Pogba, 25, ameiambia klabu ya Barcelona ya Uhispania kuwa mchezaji huyo hana furaha na maisha yake ya soka chini ya Jose Mourinho. (Mundo Deportivo, via Mail on Sunday)

Real Madrid wako tayari kutoa kiasi cha pauni milioni 200 kumnasa Eden Hazard wa Chelsea, ambaye alidokeza kuwa anataka kuondoka Stamford Bridge. (Mail on Sunday)

Real pia wako kwenye hatua nzuri ya mazungumzo na mlinda mlango wa the Blues, Thibaut Courtois, (HLN, via Sunday Express)

Chelsea imetoa ofa ya mshambuliaji wa Uhispania Alvaro Morata, 25, kwa Juventus wakati ambapo nao wanajaribu kumsajili mshambuliaji wao, Gonzalo Higuain, 30. The Blues wanadhamiria kumuuza mshambuliaji wao Olivier Giroud miezi sita tu baada ya kumnunua kutoka Arsenal. (Sunday Mirror)

Mlinzi wa Manchester United na timu ya taifa ya England, Luke Shaw, 23, amekataa kusajiliwa Everton. (Sunday Times - subscription required)


Mshambuliaji wa Wales Gareth Bale, 28, atarejea Real Madrid kwa ajili ya mafunzo siku ya Jumatatu na anatarajiwa kufanya majadiliano na meneja mpya Julen Lopetegui kuhusu mustakabali wake . (Mail on Sunday)

Napoli inaomba pauni milioni 80 kwa ajili ya mchezaji wa Senegal Kalidou Koulibaly likiwa ni jaribio la kuizuia Chelsea. (Sunday Mirror)


Arsenal inamtaka kiungo wa Juventus Rodrigo Bentancur, ambaye amewavutia alipokuwa akiwakilisha Uruguay kwenye michuano ya Kombe la Dunia. (Gazzetta dello Sport, via Daily Star Sunday)

LihatTutupKomentar