Ngoma atua Dar usiku huu Yanga wamficha kusikojulikana.


Licha ya mchana wa june 27 kutoka taarifa za mshambuliaji wa klabu ya Yanga Donald Ngoma kusaini mkataba na klabu moja huko nchini Afrika ya Kusini, ineripotiwa kuwa nyota huyo amewasili jijini Dar es Salaam usiku huu na kupokelewa na mashabiki wa Yanga.


Ngoma amepokelewa na mashabiki hao wa Yanga na kupelekwa mafichoni.

Baadhi ya wanachama wa Yanga waliofika kumpokea walionekana wako makini na kulikuwa na taarifa kwamba Simba nao walitaka kufika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambao nao walikua na nia ya  kumchukua.

Hata hivyo imeelezwa kua klabu ya Simba tayari inekwisha kufanya mazungumzo naye.
LihatTutupKomentar