LIONEL MESS AENDELEA KUANDIKA REKODI MPAA BARCELONA FC

Mshambuliaji Lionel Messi akishangilia baada ya kuifungia hat-trick Barcelona kwa mabao yake ya dakika za 26, 67 na 85 mara mbili ikitoak nyuma na kushinda 4-2 dhidi ya Sevilla kwenye mchezo wa La Liga usiku huu Uwanja wa Ramon Sanchez Pizjuan mjini Sevilla. Bao la nne limefungwa na Luis Suarez dakika ya 90 na ushei, wakati ya Sevilla yamefungwa na Jesús Navas dakika ya 22 na Gabriel Ivan Mercado dakika ya 42 na kwa ushindi huo, Barcelona inafikisha pointi 57 baada ya kucheza mechi 25, ikiizi kwa pointi 10 Atlético Madrid inayofuatia nafasi ya pili mbele ya Real Madrid yenye pointi 45 za mechi 24 

LihatTutupKomentar