HAWA HAPA WACHEZAJI WATAKAO ONGEZWA SIMBA DIRISHA DOGO

akati ikielezwa kuwa mabosi wa klabu ya Simba wapo kwenye mchakato wa kuachana na baadhi ya wachezaji ambao hawajapata nafasi ya kuonesha viwango vyao, inaelezwa pia mabosi hao wapo kwenye mkakati wa kushusha vyuma vingine katika usajili wa dirisha dogo.

Wachezaji ambao wanapigiwa upatu hivi sasa ni jina la Salum Kimenya ambaye anakipiga Tanzania Prisons ya Mbeya ambaye atatua kuchukua nafasi ya Mohammed Rashid.

Aidha, jina la kiungo Francis Kahata wa Gor Mahia FC nalo limekuwa likihusishwa zaidi tangu kumalizika kwa msimu uliopita kuna uwezekano kiungo huyo akajiunga na Simba dirisha dogo.

Ukiachana na Kahata, mipango hiyo ambayo Kocha Mbelgiji, Patrick Aussems ndiye mpikaji wa kila kitu, inaelezwa amependekeza usajili huo ufanyike ili kukifanya kikosi chake kuwa imara zaidi.

Aussems ana imani kikosi cha Simba kikikamilisha suala hilo kinaweza kufanya vema zaidi pia katika mashindano ya mechi za kimataifa ambazo zinakuja hivi karibuni.

LihatTutupKomentar