KOCHA EMMANUEL AMUNIKE AMSHANGAA SAMATTA KWA HAYA


Kocha mkuu wa timu ya Taifa Stars Emmanuel Amunike ameshangazwa na uwezo wa nahodha wa Stars Mbwana Samatta kwa kufanikiwa kuiongoza timu  kushinda kwa mabao 2-0  dhidi ya Cape Verde  kwenye mchezo wa kuwania kufuzu kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) licha ya kukosa penati.

Amunike amesema kuwa kuna ugumu kwa timu hasa katika safu ya ushambuliaji kwa kushindwa kumalizia nafasi nyingi ambazo wanazitengeneza kwa kukosa umakini.

"Wachezaji wengi wanauwezo mkubwa  wakiwa uwanjani kinachowashinda ni umakini  katika kumalizia nafasi ambazo wanazipata, nina imani  watakuwa sawa katika mchezo unaofuata.

"Mchezaji kama Samatta anaonyesha namna ambavyo anapambana, uwezo wake unaonekana hii inamaanisha kwamba Tanzania kuna vipaji vingi ambavyo vikifanyiwa kazi vitaleta matunda  kwenye taifa"alisema

LihatTutupKomentar