DREAMLINER KUWAPELEKA T-STARS CAPE VERDE,






Timu ya Taifa Stars, itasafiri na ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner kwenda nchini Cape Verde kuwavaa wenyeji wao katika mechi ya kuwania kufuzu Afcon 2019 nchini Afcon. 



Ndege hiyo itaruka kwa saa 9 bila kutua hadi nchini humo. Mashabiki wametakiwa kujitokeza kukata tiketi kwa ajili ya kwenda kuishangilia Stars. Kikosi hicho na mashabiki wake watarejea siku hiyohiyo baada tu ya mechi.



Tayari Taifa Stars imeanza maandalizi ya mchezo huo chini ya kocha Emmanuel Amunike raia wa Nigeria.



Baada ya mechi hiyo, Stars itarejea nchini mara moja kuja kujiandaa na mechi ya marudiano dhidi ya Cape Verde jijini Dar es Salaam.


LihatTutupKomentar