YANGA WAANDIKA RECORD HII HAPA


Baada ya kuchezewa soka la maana na watani zao wa jadi katika Uwanja leo, mashabiki wa Yanga wameonekana kufurahia zaidi matokeo ya suluhu bila kufungana na Simba.

Simba na Yanga zilikutana jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu Bara na mechi kumalizika kwa 0-0.

Katika kipute hicho Simba ilifanikiwa kutawala kwa kila kitu na kuwapa wakati mgumu Yanga ambao walicheza mfumo wa kujilinda zaidi na kushambulia kwa kuvizia.

Kutokana na hali hiyo, wapo baadhi ya mashabiki wa Yanga waliokuwa wakiomba vema mpira ukaaisha haswa kuelekea mwishoni mwa kipindi cha pili.

Presha iliwapa wanayanga kutokana na pasi kibao ambazo Simba walikuwa wanaichezea Yanga nusu uwanja pamoja na mashambulizi makali kuelekea langoni kwao.

Pongezi zimfikie kipa wa Yanga, Beno Kakolanya ambaye aliokoka michomo mingi langoni kwake jambo ambalo liliwapa ugumu Simba kupata matokeo.

Katika mechi hiyo, Simba ilimiliki mpira kipindi cha pili kwa asilimia 38 huku Simba ikimiliki kwa asilimia 62.

LihatTutupKomentar