LIVERPOOL NI MOTO WA KUOTEA MBALI YAICHACHAFYA PSG

Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp akishangilia na mshambuliaji wake, Mbrazil Roberto Firmino baada ya mechi kufuatia kutokea benchi na kuifungia timu hiyo bao la ushindi  dakika ya 90 na ushei ikiwalaza Paris Saint-Germain 3-2 katika mchezo wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Anfield usiku wa Jumanne. Mabao mengine ya Liverpool yamefungwa na Daniel Sturridge dakika ya 30 na James Milner kwa penalti dakika ya 36 kufuatia Georginio Wijnaldum kuchezewa rafu, wakati mabao ya PSG yamefungwa na Thomas Meunier dakika ya 40 na Kylian Mbappe dakika ya 83

LihatTutupKomentar