ANTON JOSHUA HAKAMATIKI AENDELEA KUANDIKA REKODI MPYA KILA PAMBANO



Alexander Povetkin ameshindwa kuvumilia makonde makali ya Anthony Joshua baada ya kukubali kipigo cha TKO katika raundi ya 7 ya pambano lao kali la ubingwa wa dunia uzito wa juu.

Joshua alilianza pambano hilo taratibu huku Povetkin akionekana ni hatari.

Katika raundi ya kwanza tu, Povetkin alirusha konde kali lililomtoa Joshua damu puani.

Hali hiyo ilisababisha hofu kwa mashabiki wa Joshua ambaye alianza kuongeza kasi taratibu katika raundi ya pili.










LihatTutupKomentar