YANGA YAPIGWA TENA NYUMBANI

YANGA SC imefanikiwa kufunga mabao kwa mara ya kwanza katika Kundi D Kombe la Shirikisho la Afrika, lakini ikipoteza mechi ya tatu kwa kulambwa 3-2 na Gor Mahia ya Kenya Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. 
Matokeo haya yanamaanisha Yanga inaendelea kukamata mkia katika kundi D, ikibaki na pointi yake moja iliyovuna kwenye sare ya 0-0 na Rayon Sport ya Rwanda kutokana na kufungwa mechi nyingine tatu, mbili dhidi ya Gor Mahia ukiwemo wa wiki mbili zilizopita waliochapwa 4-0 mjini Nairobi. 
Mechi nyingine ambayo ilikuwa ya kwanza kabisa, Yanga ilichapewa mabao 4-0 na USM Alger mjini Algiers nchini Algeria. 

LihatTutupKomentar