HOME BOYS VS YANGA MAPEEMA LEO

Muda wa mechi Homeboys vs Yanga leo 3 June 2018
Michuano ya Pili ya Sportpesa Super Cup ambayo inaandaliwa na Kampuni ya Michezo ya Kubahatisha ” Sportpesa” Leo inaanza rasmi huku mechi ya Kwanza ya Ufunguzi ikizikutanisha Homeboys ya Kenya watakaokabliana na Yanga kutoka Tanzania.
Yanga inashuka dimbani kucheza na Homeboys ambayo Yanga kupitia kwa Mwenyekiti wa kamati ya Mashindano Hussein Nyika amekiri kuwa hawaifahamu kabisa Homeboys lakini watahakikisha wanapata Ushindi kwani lengo lao ni kuhakikisha wanatwaa Ubingwa hivyo ni lazima washinde kila mechi.
Mechi hiyo Itaanza majira ya saa saba mchana na  tutakuwa nawe bega kwa bega kuhakikisha haupitwi na Chochote kuhusu Michuano Hiyo.
LihatTutupKomentar