FAMILIA YA MO DEWJI WATANGAZA DONGE NONO



Familia ya Mfanyabiashara, Mohamed Dewji imetangaza zawadi ya Sh bilioni moja kwa atakayefanikisha kupatikana kwake.
Mo Dewji hajulikani alipo baada ya kutekwa na watu wasiojulikana, Alhamisi iliyopita jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kwa niaba ya familia ya Dewji, Azim Dewji amesema wamedhamilia kuona mtoto wao anapatikana na wanaomba ushirikiano.
Ameishukuru serikali kwa ushirikiano na jitihada kubwa kuhakikisha Mo Dewji anapatikana.

LihatTutupKomentar