Baada ya klabu ya Mtibwa Sugar kulalamikia kutopewa fedha zake za mshindi wa Kombe la FA, Shirikisho la Soka nchini (TFF) limeibuka na kusema Mtibwa hawawezi kuzungumzia suala hilo.
Madadi ameeleza kuwa Mtibwa wamekuwa ni watu wastaarabu hivyo haamini kama wanaweza kuzungumza kwenye vyombo vya habari wakilalamikia kuwa hawajapewa fedha zao.
Mtibwa inadai kitita cha fedha ambazo ni shilingi za kitanzania, milioni 50 baada ya kufanikiwa kutwaa Kombe la Shirikisho kwa ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Singida United Juni 2 2018 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.