TETESI KUBWA ZA SOKA BARANI ULAYA LEO ALHAMIS YA SEPTEMBA 27 2018




Wachezaji wakuu kadhaa wa Manchester United wamekasiriwa na usimamizi wake meneja Jose Mourinho. Mreno huyo hivi majuzi alimuambia kiungo wa kati Paul Pogba kuwa hatakuwa nahodha wa klabu tena. (ESPN)

Pogba na Mourinho walijibizana wakati wa mazoezi siku ya Jumatano kwa sababu Mourinho alifikiri mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa alichapisha video iliyomunyesha akicheka wakati Manchester United ilishindwa na Derby katika kombe la EFL. (Sun)

Pogba aliuambia usimamizi wa United karibu miezi miwili iliyopita kuwa anataka kundoka Old Trafford. (Telegraph)

Naibu mwenyekiti wa United Ed Woodward amemuunga mkono Mourinho na hafikiri kumfuta meneja huyo mweny miaka 55. Hata hivyo wachezaji kadhaa wanataka kuhama mwisho wa msimu ikiwa Mourinho atabaki. (Star)

Kiungo wa kati Aaron Ramsey ataondoka Arsenal msimu ujao baada ya mazungumzo ya mkataba kuvunjika. Mchezaji huyo mwenye miaka 27 raia wa Wales yuko awamu ya mwisho ya mkataba wake na amehusishwa na Chelsea na pia Juventus. (Mirror)

Manchester City wanataka kiungo wa kati Muingereza Phil Foden 18, kusaini mkataba wa muda mrefu. (Mail)

Arsenal wanamfuatilia mlinzi wa Everton Ryan Astley. Mchezaji huyo mwenye miaka 16 alianza kuichezea klabu ya wachezaji wa chini ya miaka 23 mwezi Machi. (Mirror)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anasema itachuakua hadi miezi sita kwa kiungo wa kati Mbrazil Fabinho kuelewa mfumo wa kucheza wa klabu hiyo. Mchezaji huyo mwenye miaka 24 alijiunga na Liverpool kutoka Monaco msimu huu na alicheza Jumatano katika kombe la Carabao ambapo walishindwa na Chelsea. (Independent)

LihatTutupKomentar