REFA WA NAMIBIA AKATAA RUSHWA

Moja kati ya habari zilizochukua headlines leo kwenye soka la Afrika ni pamoja na hii ya refa wa Namibia kuwatia matatizoni viongozi wa soka wa Rwanda.
Refa Jackson Pavaza raia wa Namibia amewatia matatizoni viongozi wa shirikisho la soka la Rwanda FERWAFA baada ya kukataa rushwa yao ili aipendelee Rwanda katika mchezo dhidi ya Ivory Coast wa kuwania kufuzu kucheza AFCON 2019 nchini Cameroon.
Mchezo huo wa Rwanda dhidi ya Ivory Coast ulichezwa Kigali na Rwanda walipoteza kwa magoli 2-1, baada ya refa Jackson kukataa rushwa hiyo katibu wa FERWAFA, Regis Uwayezu na mkuu wa kamati ya mashindano Eric Ruhamiriza wapo chini ya ulinzi Rwanda.
LihatTutupKomentar