EDEN HAZARD APELEKA MSIBA LIVERPOOL YAONDOLEWA CARABAO

Mshambuliaji Mbelgiji, Eden Hazard akishangilia baada ya kuifungia Chelsea bao la ushindi dakika ya 85 ikiilaza Liverpool 2-1 usiku wa Jumatano Uwanja wa Anfield katika mchezo wa Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao. Hazard alifunga bao hilo baada ya kuingia dakika ya 56 kuchukua nafasi ya Willian, wakati bao lingine la Chelsea limefungwa na Emerson dakika ya 79, baada ya Daniel Sturridge kutangulia kuifungia bao zuri Liverpool dakika ya 58 

LihatTutupKomentar