TETESI ZA USAJIRI ULAYA LEO


Mchezaji wa kiungo cha mbele wa Liverpool Mohamed Salah, mwenye umri wa miaka 26, na mshambulaiji wa Tottenham na England Harry Kane, wa miaka 25, wote walikataa nafasi ya kujiunga na Real Madrid baada ya timu hiyo kuu ya Uhispania kumuuza Mchezaji raia wa Ureno Cristiano Ronaldo, kwa timu ya Juventus. (El Pais - in Spanish) 

Mashabiki wa Manchester United wamelipia bango lililo na ujumbe wa kutaka naibu mwenyekiti mtendaji Ed Woodward aondoke na litakalo peperushwa uwanjani wakati wa mechi dhidi ya Burnley Septemba 2. (Mail) 

Mlinzi wa Tottenham na England Danny Rose wanaweza kuhamishwa kwenda timu katika Ligue 1 Paris St-Germain. Mchezaji huyo mwenye miaka 28 alikataa uhamisho wa mkopo kwenda katika ligi ya Ujerumani Bundesliga timu ya Schalke msimu huu wa joto. (Evening Standard) 

Lakini Tottenham bado haijapokea ombi lolote la Rose, wala la mlinzi wa Ublegiji Toby Alderweireld, mwenye umri wa miaka 29. (Talksport) 

Tottenham itashauriana na mashabiki kuhusu eneo la kuchezea mechi yake ya awamu ya tatu ya kuwania taji la Carabao baada ya kuthibitishwa wiki hii kwamba hawatoweza kuutumia uwanja wa Wembley. (Telegraph) 

Manchester City inatafakari uhamisho wa dharura wa mkopo wa kipa wa Real Madrid Keylor Navas, mwenye umri wa miaka 31, baada ya Claudio Bravo, mwenye umri wa miaka 35 kujeruhiwa. (AS - in Spanish) 

Mchezaji wa kiungo cha kati Phil Foden, mwenye umri wa miaka 18, huenda anatarajiwa kuitwa England huku Meneja Gareth Southgate akiripotiwa kuzungumza na Meneja wa Manchester City Pep Guardiola kuhusu anavyoendelea (Sun) 

Liverpool na Borussia Dortmund zinafanya mazungumzo kuhusu mkataba wa kumsajili mchezaji wa kiungo cha mbele wa Ubelgiji Divock Origi, mwenye umri wa miaka 23. (ESPN) 
LihatTutupKomentar