JEURI YA FEDHA YAMUONDOA ANTONIO CONTE

KLABU ya Chelsea imemfukuza kocha Antonio Conte baada ya kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba kwa Pauni Milioni 9.
Klabu hiyo ilikuwa inatazama dau la kumpa Mtaliano huyo aondoke na sasa imeelekeza mawindo yake kwa Maurizio Sarri awe bosi moya Stamford Bridge huku gwiji wa klabh hiyo, Gianfranco Zola akitarajiwa kuwa namba mbii wake.
Conte amebwaga manyana Chelsea Alhamisi asubuhi na amewaaga wachezaji na maafisa wa benchi la ufundi viwanja vya mazoezi vya Cobham.
Wachezaji wa Chelsea na maafisa wa benchi wamepewa mapumziko kuanzia leo hadi baadaye wiki hii watakaporejea kwa maandaozii ya msimu mpya.
Antonio Conte amefikia makubaliano ya kuvunja mkataba wake Chelsea kwa Pauni Milioni 9
LihatTutupKomentar