LIPULI YA MUONGEZA MKATABA SHABAN ADA

TIMU ya Lipuli ya Iringa imewasainisha mikataba mipya wachezaji wake wanne ili kuwaweka mbali na klabu zinazowatamani kwa sasa.
Wakati dirisha la usajili likiwa wazi tangu Juni 15, uongozi wa Lipuli umerudi nyuma na kutazama usalama wa wachezaji wake.
Na Alhamisi Lipuli imewasainisha mikataba mipya wachezaji wake wane, beki Emmanuel Kichiba, viungo Shaabani Ada, Yussuf Mohamed na mshambuliaji, Malimi Busungu.
Shaabani Ada (kushoto)
Na Lipuli inachukua hatua hiyo ikiwa katika maandalizi ya mwanzo kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ambao utakuwa wa pili tangu ipande tena baada ya miaka mingi.
Wachezaji wote walioongezewa mikataba ni muhimu na hatua hiyo imekuja baada ya pendekezo la kocha Mkuu, Suleiman Matola ambye aliagiza watiwe pingu mapema.
LihatTutupKomentar