Samatta tayari katua Bongo

Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Ally Samatta tayari ametua nchini kuungana na nyota wengine wa Tanzania katika mazoezi yanayofanyika Uwanja wa Boko Veteran, ulioko Boko - nje kidogo ya 
jijila la Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Malawi utakaofanyika Uwanja wa Uhuru,  Jumamosi Oktoba 7, 2017 kuanzia saa 10.00 jioni. Karibu Watanzania wote kuishangilia Stars siku ya Jumamosi kujenga dhana ya mchezaji wa 12 uwanjani wakati wale 11 akiwamo Msuva, Ajib, Mbaraka wakileta faraja ya mabao
LihatTutupKomentar