HALI TETE KATIKA KLABU YA ESPANYOL WACHEZAJI 10

KOCHA wa klabu ya Espanyol ya La Liga, Abelardo Fernandez amesema kuwa mpaka sasa wana watu 10 ambao wameathirika na Virusi vya Corona.

 Katika  wagonjwa hao 10, wachezaji nane wa kikosi cha kwanza  nao wamekuwa ni kati ya watu kumi ambao wameambukizwa Virusi vya Corona.

 Wachezaji  nane wa kikosi cha kwanza pamoja na  makocha wawili ndiyo ambao wamepata maambukizi ya Virusi vya Corona.

 Kocha huyo amesema: “ Ndani ya klabu ya Espanyol tuna kesi 10 za maambukizi ya Virusi vya Corona , wachezaji nane wa kikosi cha kwanza na makocha wawili.

“Mambo ni magumu kutokana na hali halisi ya sasa  na hatujui hata  hatma ya ligi ikoje na hapa tulipofika hata ligi ikirejea bado hali za wachezaji hazijawa sawa na kila mtu anatamani kurudi uwanjani," amesema.

LihatTutupKomentar