LIVERPOOL YAANZA KWA KISHINDO

Mshambuliaji Mohamed Salah akiifungia Liverpool bao la pili dakika ya 19 baada ya Grant Hanley kujifunga dakika ya saba katika harakati za kuokoa krosi ya Divock Origi kuwapatia Wekundu hao bao la kuongoza katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Norwich City kwenye mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Anfield. Mabao mengine ya Liverpool yalifungwa na Virgil van Dijk dakika ya 28 na Origi dakika ya 42, wakati la Norwich City iliyorejea Ligi Kuu msimu huu lilifungwa na Teemu Pukki dakika ya 64

LihatTutupKomentar