BEKI SIMBA ATOA ONYO KWA TIMU ZINAZO SHILIKI LIGI KUU _(TPL)

Beki wa kulia wa Simba, Zana Coulibaly ambaye amesaini leo kandarasi ya miaka miwili na kupewa jezi namba 21 amesema kuwa amekuwa akiwasikia wapinzani wa timu yake Yanga hivyo anajipanga kuweza kuonesha maajabu.

Beki huyo ambaye amesajiliwa ili kuziba nafasi ya beki Shomari Kapombe ambaye amefanyiwa operesheni ya enka ya mguu baada ya kupata majeruha alipokuwa na timu ya Taifa ilipokuwa kambini nchini Afrika kusini, leo ameanza mazoezi na kuonyesha kasi akiwa uwanjani.

"Ninaamini Yanga ni timu bora yenye wachezaji wazuri na kazi kubwa itakuwepo mara nitakapokutana nao, mchezo huo utakuwa na ushindani mkubwa kutokana na upinzani uliopo," alisema.

Coulibaly ni raia wa Burkina Faso ametokea klabu ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast alishuhudia Simba wakitakata mbele ya Mbabane Swallows siku ya Jumapili kwa kupata ushindi wa mabao 4-1, ana umri wa miaka 26.

LihatTutupKomentar