TETESI KUBWA ZA SOKA BARANI ULAYA LEO JUMATANO YA SEPTEMBA 26 2018



Rais wa Real Madrid Florentino Perez anaamini mshambuliaji wa Ureno Cristiano Ronaldo, 33, siku moja atarudi katika klabu hiyo. Ronaldo alijiunga na Juventus mwezi Julai baada ya miaka tisa huko Bernabeu. (ESPN)

Ronaldo na mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi, 31, wamejikuta kwenye mzozo baada ya kukosa kufika kwenye sherehe za tuzo za Fifa. (Marca via Express)

West Brom wanatarajiwa kumsaini wing'a wa zamani wa Crystal Palace Bakary Sako, 30, wiki hii. Mchezaji huyo wa kimataifa raia wa Mali amekuwa bila ajenti tangu akatae ofa ya mkataba kutoka Palace. (Sky Sports)

Arsenal wanammezea mate wing'a wa Rennes mwenye miaka 20 raia wa Senegal Ismaila Sarr ambaye amefananishwa na mchezaji wa Barcelona Ousmane Dembele. (Mirror)

Mmililki wa Chelsea Roman Abramovich anahitaji sio chini ya pauni bilioni 3 kuweza kuiuza klabu hiyo. (Bloomberg)

Msaidizi wa Chelesea Gianfranco Zola anaaminia wing'a Mbelgiji Eden Hazard, 27, hajafikia kiwango chake cha juu zaidi na anaweza kuwania tuzo za juu kwenye kandanda. (Telegraph)

Mkurugenzi wa kiufundi wa shirikisho la FA Dan Ashworth, 47, yuko kwenye mazungumzo kuhusu wajibu kama huo uko Brighton. (The Guardian)

Mlinzi wa zamani wa Liverpool Jamie Carragher ameunga mkono uamuzi wa mlinzi Declan Rice 19, wa kukataa ofa ya mkataba huko West Ham. (Talksport)

Mmiliki wa Monaco Dmitry Rybolovlev anataka kuiza klabu na kuna ripoti za wanunuzi kutoka Marekani na UAE. (le10sport.com - in French)

LihatTutupKomentar