BARCELONA HAIKAMATIKI LALIGA

Lionel Messi akifurahia baada ya kufunga mabao mawili dakika za 16 na 61 Barcelona ikishinda 8-2 dhidi ya Huesca iliyopanda La Liga msimu huu jana Uwanja wa Camp Nou. Mabao mengine ya Barca jana yamefungwa na Jorge Pulido aliyejifunga dakika ya 24, Luis Suarez mawili dakika za 39 na 90 na ushei kwa penalti, Ousmane Dembele dakika ya 48, Ivan Rakitic dakika ya 52 na Jordi Alba dakika ya 81, wakati ya Huesca yamefungwa na Cucho Hernandez, anayecheza kwa mkopo kutoka Watford dakika ya tatu na Alex Gallar dakika ya 42

LihatTutupKomentar