YANGA NA YOUTHE ROSTAND WAVUNJA NDOA YAO

Uongozi wa Yanga umetangaza kiachana na golikipa Youthe Rostand raia wa Cameroon baada ya pande mbili kukubaliana kuvunja mkataba.
Ofisa habari wa Yanga Dismas Ten amesema Rostand klabu hiyo ilikuwa tayari kumtoa kwa mkopo kwenda African Lyon lakini golikipa huyo hakuwa tayari.
“Golikipa Rostand hayupo Morogoro kwa sababbu tayari makubaliano ya pande mbili (mchezaji na klabu) yamefikiwajuu ya kusitisha mkataba wake.”
“Klabu ilikuwa na mpango wa kumpeleka kwa mkopo African Lyon lakini yeye mwenyewe kwa sababu zake za kiafya alisema hayuko vizuri sana ‘ki-saikolojia’ kwa hiyo anahisi hawezi kuitumikia Yanga kwa 100% akaomba klabu ifanye makubaliano ya kusitisha mkataba.
“Jambo hilo limekubaliwa, kinachosubiriwa sasa ni yeye kupatiwa stahiki zake ili aende akapumzike na kufanya taratibu nyingine za maisha akiwa nyumbani kwao.”
“Rostand atalipwa stahiki zake, pesa ya usajili iliyobaki na mishahara ambayo alikuwa hajapata katika kipindi cha hivi karibuni, ndio makubaliano yaliyofikiwa na baada ya hapo ataondoka kwenda kuanza maisha mengine.”
LihatTutupKomentar