WACHEZAJI 8 WAIACHA YANGA

aada ya kuleta takribani wachezaji 14 kutoka nje ya nchi waliokuja kufanya majaribio na kikosi cha Yanga nchini, jumla ya 8 wameondoka na 6 wakibakia.

Meneja Mkuu wa timu, Hafidh Saleh, amesema kwa sasa wamebaki na wachezaji 6 pekee huku wengine wakifeli mazoezi ambapo sasa watakuwa wanarejea makwao.

Saleh amesema wachezaji waliofeli wameondoka kutokana na mchujo unaoendelea kwa ajili ya kupata wale wanaohitajika kwa ajili ya kukisuka upya kikosi.

Ikumbukwe siku kadhaa zilizopita, Yanga ilitaka kuleta wachezaji 14 wa kimataifa kwa mujibu wa Ofisa Habari wa klabu, Dismas Ten kwa ajili ya kufanya majaribio.

Kikosi hicho kipo kambini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Gor Mahia FC ya Kenya na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.
LihatTutupKomentar