SIMBA YAPORA MCHEZAJI KUTOKA RWANDA WAO WADAI KUIPELEKA FIFA

Imeripotiwa kuwa uongozi wa klabu ya Kiyovu kutoka Rwanda umetishia kwenda FIFA kwa madai ya mchezaji wake, Fabrice Kakule, kuonekana na timu ya Simba akifanya mazoezi jijini Dar es Salaam.

Taarifa kutoka Rwanda zinaeleza kwa mujibu wa Rais wa Kiyovu, Jean Pierre, amesema atafanya mipango ya kupeleka mashtaka FIFA akieleza kuwa Kakule bado ana mkataba na Kiyovu ambao unamaliza mwaka kesho.

Pierre amefunguka akiwataka Simba ni vema wakakutana
kufanya makubaliano juu ya mchezaji wake badala ya kumsajili kinyemela, jambo ambalo linaenda kinyume na tataribu za usajili wake.

Inaelezwa kuwa Kakule atakuwa anamaliza mkataba wake mwishoni mwa mwezi Julai mwaka kesho hivyo Pierre amewataka Simba kumuachia mchezaji wake mara moja au wakae mezani ili waweze kumalizana.

Kakule tangu awasili nchini amekuwa akifanya mazoezi na mabingwa hao wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2017/18 ambacho kipo katika mashindano ya KAGAME yanayoendelea hivi sasa jijini Dar es Salaam.
LihatTutupKomentar