KUIONA YANGA VS RAYON SPORTS BUKU 3


Jumatano May 16 kutakuwa na mchezo wa Kombe la Shirikisho barani Afrika hatua ya Makundi kati ya Yanga wenyeji uwanja wa Taifa dhidi ya wageni rayon Sports ya Rwanda.
Mchezo huo Umepangwa kuchezwa majira ya saa moja Usiku, Huku Viingilio vya mchezo huo vikitajwa kuwa ni
VIP A 15,000 ,
VIP B na C 7000
PS 3000.
Yanga watashuka katika mchezo huo ikimkosa Kiungo wake Said Juma Mkapu ambaye anakadi 2 za Njano na Kanuni za Mashindano zikizuia mchezaji mwenye kadi 2 za Njano kucheza mchezo unaofuata.

LihatTutupKomentar